Walimu Hewa

Walimu Hewa

Walimu Hewa

Jambo la "Walimu Hewa" haliko tu barani Afrika lakini athari ya kuwalipa kwa walimu ambao hawapo, hawaingii kazini au ambao wana vyeti gushi ni kubwa sana hasa kutokana na wingi wa wanafunzi darasani, uhaba wa walimu na kwamba mishahara huwakilisha 80% ya bajeti za elimu katika kanda. 

Katika miaka ya hivi majuzi kumekuwa na ripoti za ulaghai mkubwa wa 'walimu hewa' katika nchi nyingi na makadirio kuweka gharama ikiwa zaidi ya bilioni $20 kila mwaka. Hebu fikiri kama pesa hizo zilitumika kwenye rasilimali muhimu badala yake. 

Katika warsha za ESSA na wanafunzi na walimu kote barani Afrika kuna ujumbe mkubwa na wa wazi kutoka kwa washiriki "Tafadhali tusaidie kutafuta njia za kupunguza ulaghai huu na kuwazuia watu hawa kuiba hatima zetu!"

Nchini Liberia, mpango amilifu unaojumuisha hatua mbalimbali zilizoweza kuhifadhi fedha za kutosha kuwaajiri walimu 2,000 wapya. Mabadiliko kwenye mifumo ya malipo, michakato ya kuajiri na vilevile menejimenti ya shule na michakato ya ukaguzi inaweza kusaidia.

Mwaka wa 2017, ESSA ilianza mradi wa kuelewa tatizo hili kwa undani zaidi na kukusanya maarifa kutoka kwa wale ambao wamefanya kazi kwa uamilifu na mafanikio ili kupunguza kiwango cha aina hii ya ulaghai katika nchi zao. Mwaka wa 2018 tutapeleka mradi huu hadi awamu inayofuata. Kaa chonjo!